Monday, February 4, 2013

HALI YA MATUMAINI BADO NI MBAYA...ZOEZI LA KUMRUDISHA HALIJAFANIKIWA BADO


Waigizaji zaidi ya 30 ambao jumapili february 3 2013 walijitokeza kumpokea mwigizaji mwenzao mgonjwa Matumaini, walirudi mikono mitupu baada ya mwigizaji huyo aliekua anatarajiwa kuwasili Tanzania akitokea Msumbiji kushindwa kufanya hivyo chanzo kikiwa ni hati yake ya kusafiria ambayo akiwa uwanja wa ndege aliagizwa kuishughulikia kwenye ofisi za uhamiaji ambazo zipo mbali na uwanja wa ndege.
.
Matumaini amekua Msumbiji kwa wiki kadhaa alikokwenda kufanya show lakini muda mfupi baadae mambo yakageuka na kuanza kuumwa miguu, mwigizaji huyu anatarajiwa kuwasili Dar jumanne au jumatano na tayari umoja wa waigizaji umepanga kumpeleka hospitalini moja kwa moja.
Waigizaji waliokwenda kumpokea.

No comments:

Post a Comment

TOA MAONI YAKO HAPA