Thursday, January 24, 2013

WANAFUNZI WA CHUO CHA ST. JOHN'S WAANDAMANA KUPINGA VITENDO VYA UBAKAJI WANAVYOFANYIWA

Ni mchaka mchaka ulioendana na nyimbo za hisia





Msafara hapa unaelekea maeneo ya Bungeni

Kila walipopita walikuwa wakishindikizwa na polisi kuhakikisha amani inatawala



Gari la maji ya kuwasha lilikuwepo lakini wanafunzi hao hawakutishika na kitu chochote kile kutoka kwa Polisi

Wanafunzi walifika mpaka Nyerere Square waliimba nyimbo mbalimbali mahala hapo




Baada ya kutembea mji mzima na mabango yao na kuhakikisha kiu yao imekwisha basi waliamua kurudi chuoni

Gari la washa washa nalo lilikuwepo lakini watu walikuwa na jaziba zao vilevile mwanzo mwisho

Barabara zilikuwa zimetawaliwa na wanafunzi kwa kiasi kikubwa, mpaka kusababisha magari kutopita

Hapa ilibidi nipande gari la polisi ili niweze kuchukua picha vizuri, sio siri polisi wenyewe walikuwa wamechoka kwa kutembezwa mji mzima baada kuchat nao kwenye gari ilo

Hapa ndipo safari ya maandamano ilipoanzia na ndipo safari hiyo ilipoishia maeneo haya ya kwenye bendera mbele ya jengo la administration.

Safari ya maandamano ya amani ikawa imeishia chuoni hapo baada ya kuona kuwa ujumbe wao umefika. Wanafunzi wa chuo wamechoshwa na matendo mabaya ambayo wanafanyiwa ikiwa ni pamoja na kubakwa, kulawitiwa, kuibiwa vitu vyao kama Laptop na vitu vingine. Wameonesha umoja wao kwa sababu ya kuchoshwa na mambo hayo, ambapo leo asubuhi kuna wanafunzi walivamiwa na kuibiwa Laptop. Hivyo wakaamua kujikusanya asubuhi hiyo hiyo mida ya saa kumi na mbili alfajili na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja ambaye walimpiga na baadae kuchukuliwa na polisi.

No comments:

Post a Comment

TOA MAONI YAKO HAPA